Posts

KACOU 75: TULIONA NYOTA YAKE

(Ilihubiriwa Jumapili Asubuhi, Juni 1, 2008 huko Adjame kasha huko Anyama, karibu na Abidjan – Ivory Coast) 1 Akina ndugu, jueni kwamba Ukristo wa awali unaweza tu kuwa kurudi Edeni, ambako mwanadamu alianguka ili kumwinua milele! Hapo mwanzo, haikuwa mitala! Mungu alichukua ubavu mmoja tu kutoka kwa Adamu na kwa ubavu huo, akamfanya mwanamke moja na nyoka alipomwaibisha, Mungu hakuthubutu kubadilishia au kumuumbia Adam mwanamke mwingine ! Lakini mitala imetajwa katika Mwanzo 4 kuwa ni moja ya matendo ya wana wa shetani duniani.  2 Angalia jozi hizi za njiwa, jozi hizi za wanyama, maumbile yote yanafundisha kwamba kuoa wanawake wengihaikuwa taasisi ya asili ya Mungu! Ni mjukuu wa Kaini aliyefanya hivi! [Ndl: Kusanyiko linasema: “Amina! "]. Unaweza kuja hapa na wake wawili au watatu, lakini mara tu umejua Ujumbe huu na kupokea ubatizo wako, huwezi kuwa na wake wawili tena. Na kama ndugu akifanya hivyo, hawezi kamwe kukubaliwa katika Ujumbe huu hata miaka kumi au ishirini kutoka sas...

KACOU 80: JE NABII HUZUNGUMUZA KWA AJILI YA NABII MWINGINE?

(Ilihubiriwa Alhamisi jioni,O ctoba 09, 2008 huko Anyama, karibu na Abidjan- Ivory Coast) 1 Vizuri sana,  nina  maswali kadhaa nataka kujibu.  Swali la kwanza ni: “Ndugu Philippe, wakati wa jioni uliisha wakati  Malaika wa Aprili 24, 1993 aliposhuka na tunajua kwamba wote walioishi tangu 2002 wako chini ya mamlaka ya Mathayo 25: 6.  Sasa kwa waliokufa kati ya 1965 na 2002 itakuwaje?  2  Jibu ni kwamba wote walio kisha kuamini na kubaki waaminifu kwa Ujumbe wa William Branham na waliokufa katika matarajio na matumaini ya Kelele ya usiku wa manane wameokolewa!  Wale waliongoja tafsiri ya lugha isiyojulikana ya Sabino Canyon au jiwe jeupe kulingana na mapendekezo ya William Branham katika ndoto ya Junior Jackson!  3 Iko kwenye brosha: "Je,hii ni ishara ya mwisho, bwana?  ambayo nitasoma kidogo ... "... Maji, yalipokuwa yakitiririka, yalikuwa yamechora aina za herufi kwenye mawe haya, nawe ulikuwa pale, ukitafsiri kile kilichoandikwa kwenye ...

KACOU 79: KUNYIMWA VISA NA MARUFUKU YA KUSAFIRI

(Ilihubiriwa Alhamisi jioni, Septemba 04, 2008 huko Anyama, karibu na Abidjan – Ivory Coast) 1 Niliposikia kuwa faili langu la ombi la viza lilipelekwa Ubelgiji ili kuchunguzwa na viongozi wa Ubelgiji, nilitarajia chochote na nilipoona kwamba ilichukua muda mrefu, nilianza kuelewa!  Mimi si mwanasiasa na sijawahi kushirikiana na mtu yeyote na faili yangu ya kuomba viza ilipelekwaje Ulaya?  Japo, hatujasikia kamwe walimkatalia mchungaji viza. 2 Baadaye, nilipokea simu kutoka Ubelgiji ikiniambia kwamba walinikatalia visa! Na kwamba ni Abidjan ndio inapaswa kunieleza sababu!  Nilisema ndani mwangu : Iwe hivyo, lakini sio wavuta sigara wanaopaswa kusema kwamba mimi ni nabii wa kweli au wa uwongo!   3 Waliowachagua wameshasema kwamba mimi ni nabii wa uongo na najua amtasema vinginevyo!  Ila tu, Ivory Coast, makanisa yake na wakaaji wote wa dunia wanipende kabla ya kuniua!  Hata wakininyima viza mara elfu moja, hiyo haitaniondoa chochote kwa kile niko au nin...

KACOU 78: ISHARA ZA KUJA KWAKE

(Ilihubiriwa Alhamisi jioni, Agosti 21, 2008 huko Annyama, karibu na Abidjan – Ivory Coast) 1 … Vema!  Mungu awabariki!  Nina mfululizo wa maswali hapa ambayo nataka kujibu.  La kwanza ni: “Ndugu Philippe, tunajua kwamba Malaika wa Aprili 24, 1993 ni yule wa Ufunuo 19 lakini je, malaika huyu yuko pamoja na nabii au ndani ya nabii?  » 2 Ndiyo, hasa, Malaika wa Aprili 24, 1993 ni yule wa Ufunuo 19 na malaika huyu ni udhihirisho wa Bwana Yesu Kristo.  Uelewa mzuri ni kwamba malaika huyu yuko pamoja na nabii kama ilivyokuwa kwa Musa, William Branham na manabii wengine wengi.  Anaweza kuwa mbali nao, karibu sana nao au wakati fulani, kujiimarisha ndani yao kimwili ikiwa ni lazima, kwa kusudi maalumu.  3 Jambo muhimu zaidi ni kujua wakati ni malaika na wakati ni ndugu!  Wakati wao ni watu wawili tofauti na wakati mwingine ni mtu mmoja!  Na katika huduma ya kurejesha upya, ni lini kipindi cha simba, kipindi cha ndama, kipindi cha tai, au kipindi cha...

KACOU 76: NEEMA ILIYOTOLEWA AFRIKA

(Ilihubiriwa Jumapili asubuhi, Juni 15, 2008 huko Anyama karibu na Abidjan – Ivory Coast) 1 Kama kwa mataifa mengine ya dunia, Mungu ametoa neema kwa Afrika.  Lakini kabla ya mahubiri, ningependa kuanza na maelezo.  Ni kuhusu mahubiri. Natamani  kwenye ibada za jioni au kwenye moja ya ibada ya jioni kwa wale walio  wawili au watatu, mahubiri yawe kulingana na chaguo la mhubiri au mchungaji yasomwe na atoe maoni yake anaposoma. 2 Vema!  Mtu ambaye alisikiliza mahubiri "Tuliona nyota yake!"  akasema, "Ndugu Philippe , waandishi bado waliwajulisha Mamajusi kwamba Mfalme wa Wayahudi atazaliwa Bethlehemu!"  "Nilisema hapana!  Mamajusi hawakuhitaji!  Ilikuwa nzuri tu kwa Herode na Wayahudi.  Waandishi, licha ya mstari huu, hawakuweza kujua ni yupi kati ya watoto wote waliozaliwa wakati wa miaka miwili alikuwa Kristo!  Na hakuna mstari ungeweza kuelekeza nyumba ila nyota ndio ilionyesha!  [Mhr: Kusanyiko linasema, Amina!  ”]....

KACOU 73: WAUZAJI WA NAFSI

(Ilihubiriwa Jumatano jioni Februari 27, 2008 Ayopougon – Koweit, Abidjan – Ivory Coast) 1 ... Niruhusu niwafikishie salamu za Dada Mireille wa Ubelgiji.  Pia, nilimwomba Mchungaji Akobe kunakili mahubiri “Shibolethi au athari ya damu”.  Alimaliza.  Nitasoma na mutakuwa nayo hivi karibuni! 2 Pia ninaomba kwamba unaweza kutoa michango kwa Ndugu Boga Éric na kwa Ndugu Yanick Aka, ambao wamejitolea kwa Ujumbe huu na ambao wanajali kila siku wale wote walio nje.  Unajua kwamba wana familia wanazoziongoza na kwamba wamejitolea kabisa kwa huduma hii lakini hawana chanzo cha mapato. 3 Vema!  Sasa ningependa kujibu maswali mawili.  Kuna kadhaa, lakini ningependa kujibu mawili kati yao.  La kwanza ni: “Ndugu Philippe, katika Ufunuo 18:10-13, je, roho za watu ni sehemu ya bidhaa ambazo Kanisa Katoliki lilikuwa likiuza?  Hili liliwezekanaje?  Tunawezaje kuuza roho za watu kwa pesa?  ".  Na hilo ndilo litakalokuwa somo la mahubiri yangu jioni y...

KACOU 72: MAAGIZO JUU YA UINJILISTI

(Ilihubiriwa Alhamisi 08 Mei, 2008 huko Anyama, karibu na Abidjan – Ivory Coast) 1 Nataka kutoa maagizo juu ya uinjilisti, lakini mniruhusu nizungumzie baadhi ya mambo!  [Ndl.: Kusanyiko linasema: Amina!]. 2 Kwa wale ambao hawaelewi ninachosema kuhusiana na William Branham, jueni kwamba naamini kabisa kwamba William Branham ni nabii wa kweli aliyetumwa na Mwenyezi Mungu, kulingana na Malaki 4 na Ufunuo 10:7 na kwamba hata Maneno yake yana thamani sawa na maneno ya manabii wa Biblia, lakini siamini kwamba miaka kumi baada ya kifo chake, mmoja wa wale waliomfuata angeweza kupeleka nafsi moja Mbinguni.  Ujumbe wake ulikuwa wa wakati fulani na wakati huo umepita, zaidi ya miaka 40.  [Ndl.: Kusanyiko linasema: Amina!]. 3 Kuhusu maelfu ya vipeperushi vinavyosambazwa ulimwenguni kote kutoka Ulaya, nadhani ilikusudiwa tu kuandaa jukwaa kwa ajili ya huduma tukufu chini ya hema na kupitia hilo, ujio wa pili wa Bwana Yesu Kristo kama alivyojulisha mwenyewe katika Mihuri Saba.  ...