Posts

Showing posts from May, 2024

Kacou 162: Noti kwa mwisho wa Ujumbe wa Mathayo 25:6

(Maneno ya mwisho ya Ndugu Philippe kufuatana na mwisho wa Ujumbe wa Mathayo 25:6) 1 Kaka na Dada, Jumamosi hii, Mei 11, 2024, mimi, Ndugu yenu Philippe, nawatumia, kwa noti hii, maneno ya mwisho ninayotamka kufwatana na utume wa Mathayo 25:6 ambao nilikabidhiwa Aprili 24. 1993. Mnamo Januari 21, 2024, nilipopaza sauti: “pandeni wote kwenye chumba cha juu!  ", Sikujua kwamba mimi pia ilibidi ninyamaze na kukomesha misheni yangu.  2 Ujumbe wa Mathayo 25:6 umekamilika.  Na ni kwa ruhusa ya  Mungu ninawajulisha maneno haya ya mwisho.  Sasa ni kwa yule ambaye Mungu atamkabidhi mwenge kutuingiza katika uamsho wa wanawali kumi.  Lakini hilo halinizuii kuwatembelea ninyi ikiwa Mungu ataniruhusu, kwa sababu ninawapenda na nina hilo moyoni mwangu.  3 Tunapohubiri na kudumu katika Ujumbe wangu, hebu sasa na tujingojee kwa mtu huyu mwengine na hatua hii inayokuja.  Lengo la Ujumbe wangu halikuwa kuwaongoza kwangu ila kuwaongoza kwa Mungu.  Kuanzia sasa,...

KACOU 64: TAFSIRI YA MAONO MAWILI

(Ilihubiriwa Jumatano jioni, Oktoba 17, 2007 huko Adjame, Abidjan – Ivory Coast) 1 Wakati nabii mjumbe anahudumu duniani, Mungu hutayarisha mazingira na wengi wa wale ambao majina yao yaliandikwa katika kitabu cha Uzima cha Mwana-Kondoo kabla ya kuwekwa misingi ya ulimwengu huanza kuzaliwa duniani. 2 Vema!  Napenda kuzungumza juu ya kitu kingine kabla ya kuanza. Malkia wa Sheba alipokuja kwa Sulemani, angalieni, kuhusu hekima ya Sulemani, Biblia inasema kwamba yeye mwenyewe alikuwa na hekima nyingi na hata kufikia hatua ya kumjaribu Sulemani kwa mafumbo na vitandawili.  2 Mambo ya Nyakati 9. Na kuhusu mali ya Sulemani, Biblia pia inasema kwamba alimletea manukato mengi na kundi kubwa la ngamia ndiyo waliyoibeba.  Alitoa zaidi ya tani tatu za dhahabu kwa Sulemani.  Hakuna mtu aliyekuwa ametoa dhahabu nyingi sana kwa Sulemani.  Alimletea mawe ya thamani kwa wingi sana.  Mnaona? 3 Mungu awabariki!  Jioni ya leo, natamani kusoma kwanza maono ya Aprili 24, ...

KACOU62: WEWE NI NANI BWANA ?

(Ilihubiriwa Jumatano jioni, Mei 30, 2007 hukoAbobo, Abidjan – Ivory Coast) 1 Nikizungumza juu ya kutokosea, nilisema kwamba inapaswa kuonekana kama muhuri, ikimaanisha kama alama ya posta  au stempu ;  hiyo ni kusema, kabla nabii hajaja kwenye huduma, Mungu anaweka alama juu yake, Anaandika juu yake: "asiyeweza kukosea".   2 Kwa hiyo hata afanye nini au atasema nini, yeye hakosei.  Na Mungu anaweza kuruhusu mambo kutenganisha magugu na ngano, lakini hilo halitaathiri kutokosea kwa nabii huyo. Mnaona ?  Hivi ndivyo na hii ndiyo sababu Biblia haiandiki kamwe maisha ya nabii mjumbe.  Biblia inasema mfalme fulani alifanya lililo jema au baya machoni pa Bwana, lakini unawezaje kusema kwamba nabii mjumbe hakwenda sawasawa mbele za Mungu?  Mnaona ? 3 Vema!  Sasa hebu tuchukue Biblia zetu kutoka katika kitabu cha Matendo ya Mitume.  Matendo sura ya 9 na tusome mistari mitano ya kwanza.  “Lakini Sauli, akieendelea  kuwatia hofu na kuwa...

KACOU 60: FILAMU YA HUKUMU YA MWISHO

(Ilihubiriwa Jumapili Machi16, 2003 huko Locodjro, Abidjan – Ivory Coast) 1 Vema! Hebu tuchukue Biblia zetu!  Nitasoma Mathayo 23:34-35 kisha nitasoma Ayubu 33:23-24 nitakayozungumzia wakati ujao.  Tusome katika Mathayo 23: “Ndio maana, tazameni, mimi nawatumia manabii, na wenye hekima, na waandishi;  na mtawaua na mtawasulubisha, na mtawapiga mijeledi katika masinagogi yenu, na mtawatesa kutoka mji hadi mji, ili damu ya wenye haki wote  iliyomwagwa duniani ihanguke juu yenu, kuanzia damu ya Abeli mwenye haki, hadi damu ya Zekaria, mwana wa Barakia, ambaye mlimwua kati ya hekalu na madhabahu."   2 Tusome pia Ayubu 33:23-24: “Ikiwa yuko mjumbe kwake, mfasiri, mmoja katika elfu, ili kumwonyesha mtu kile ambacho ni haki kwake, atamrehemu, na atasema Mwokoe ili asishuke shimoni; nimepata upatanisho. "Amina!  Mtafakari juu ya andiko hili ya Ayubu 33, nitarudi kwa hili kama ninavyorudi kwenye Mathayo 23 leo. 3 Bila shaka, Nimesoma katika kitabu cha Mtakatifu...

KACOU 59: MAANAYA UJUMBE WA WAKATI

(Ilihubiriwa Jumapili asubuhi , Tarehe  14 Mei 2016, Pale Abobo, Abidjan – Ivory Coast ) 1 Je, "Ujumbe wa wakati" unamaanisha nini?  Ni kuhusu hilo nataka kuzungumza leo.  Lakini kabla ya hilo, nina maelezo kadhaa.  Anayeongoza kuungama hadharani lazima awe wa kiroho.  Kwa sababu, katika kesi zenye upinzani na nyinginezo, yeye ana neno la mwisho kama refarii katika uwanja. 2 Na kwa ajili ya uingiliaji kati wa maungamo, mtu huingilia kati katika kusanyiko wakati uingiliaji kati huu unaimarisha kusanyiko zima.  Vinginevyo, mtu anaweza kumpa nasaha ndugu yake baada ya ibada.  Ikiwa mara kwa mara uingiliaji  wa ndugu haaujengi kutaniko, acha anyamaze milele. 3 Pia, nimetoka tu kupata toleo la Kiingereza la Darby, toleo la 1884 na nikaenda moja kwa moja kuona inachosema katika Ufunuo 12:18 na nikapata kwamba hakuna mstari wa 18 kwenye Ufunuo 12 na mstari wa kwanza wa Ufunuo 13 ni: ….. 4 Hebu nisome Ufunuo 13:1: “Nami nikasimama juu ya mchanga wa bahari...